Na mwandishi wetu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi amewatembelea Wajane wa viongozi mbalimbali akiwemo wa aliyekuwa Muasisi wa Mapinduzi Marehemu Hafidh Suleiman Almasi , Mjane Bi Mtumwa Suleiman Farhan nyumbani kwake Kilimani Juu , Mkoa wa Mjini Magharibi .
Pia amemtembelea Mjane wa Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Aboud Jumbe Mwinyi, Mjane Fatma Mohamed Hassan nyumbani kwake Mombasa kwa Mchina, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 03 Mei 2024
0 Comments